MELANIA (najutia kukupoteza)
JIFUNZE kabla dunia haijakufunza, Naomba nikubali Kuwa duania ni malimu mzuri snaa kWa watoto Wakaidi na wasiosikia Kama Mimi 🥹💔.
Dunia imenifunza pakubwa sana.
Niite Kenzo, mwanaume ambaye nilikuwa na Bahati sana, mwanaume ambaye nilitengewa chakula Chema kabisa na Mungu lakini kwakuwa nilikuwa a kiburi cha pesa bıkalım wags kWa kuamini Kuwa kila kitu ni pesa lakini dunia ikaja kuninyoosha.
Unataka kujua ni kitu gani kilinikuta baada ya kupuuzia baraka za Mungu ? TUKUTANE NDANI UA KISA CHETU İKİ.
MELANIA (najutia kukupoteza)
MTUNZI: PATRICIA DAMAS
SEHEMU YA: 01
www.tupohapa.com
ANZA NAYO…..
🤍🤎🤍🤎🤎🤍🤎🤍
Yooooh WhatsApp, KENZO hapa Mtoto wa Tajiri mkubwa sana hapa jijini dar es salaam, Kijana ambaye nikiingia sehemu yoyote ile lazima wanawake wapapatike kutokana na muonekano lakini pia na kumwaga pesa.
Nyumbani kwetu tumezaliwa watoto wawili tu Yaani Mimi na dada yangu, halafu Mimi ndio last born.
Kiukweli mzee wetu ni mtu Mwenye upendo sana, Mara nyingi uwa nasema kuwa upendo na misaada anayotoa baba yangu ndio inamfanya anafanikiwa kila hiitwapo Leo.
Mimi ni msomi Bwana na sijawai kusoma hizi shule za kula ugali maharage Wala makande.
Baba yangu alihakikisha Kuwa sisi watoto wake tunAsoma shule nzuri na tunaishi maisha mazuri ambayo yeye anataka sisi tuishi.
Ukiachana na maisha mazuri, wazazi wetu walihakikisha Kuwa sisi watoto wao tunaishi kwenye maisha Fulani hivi ya huruma, kujiheshimu, kujipenda lakini pia na kuwapenda wengine.
Akili Mbiu ya baba yangu Nyumbani ilikuwa ni kulinda reputation ya familia, Yaani baba yangu na ujinga ni vitu viwili tofauti.
Kenzo Mimi Bwana Naomba nikubali Kuwa familia yangu hainifahamu, Yaani hainijui kabisa, Yaani Kenzo wanayemjua wao na huyu Kenzo ambaye naishi ni vitu 9 tofauti.
Nyumbani kwetu Mimi nilikuwa ni Kama malaika wa nidhamu vile lakini ukija uku kwenye pande zangu weeeeeh 😂🙌 utajua ujui.
Niliishia maisha yangu kwa kuhakikisha Kuwa familia yangu haitambua mambo ya hovyo ninayoyafanya nje ya Nyumbani.
Hapa nyumbani kwetu Bwana, kuna aka kasichana Kanaitwa MELANIA. Melania nimemfahamu tangu sote tukiwa darasa la 7 kwani ndio kipindi ambacho MELANIA na mama yake waliamia pale Nyumbani.
Mama mzazi wa MELANIA alikuwa ni house girl wetu, na kwakuwa hakuwa na sehemu ya kukaa baada ya mume wake kufariki, baba akaamua kumpatia mama MELANIA Nyumba yetu ndogo ya nje ili awezi kukaa na Binti yake.
Maisha yalisonga uku mama akiwafanya MELANIA na mama yake Kuwa ni sehemu ya familia yetu.
Tulipofika kidato cha nne tuliweza kufanya mtihani yetu na kwa Bahati mbaya MELANIA hakuweza kufaulu na hii ilimpa huzuni snaa mama yake ambaye alikuwa akiitaji Mtoto wake Kuwa msomi Sanaa.
Baba yangu alimpa Melania chance ya kumsomesha lakini MELANIA akakata kwa kusema.
“Kiukweli mimi siwezi kurudi shuleni kwa sasa, sababu kuu ni kuogopa kuwapotezea muda lakini pia kupoteza pesa zenu , Kiukweli sikuwai kuelewa uko darasani”
“Unapendelea kujifunza nini ??”
Baba alimuuliza Melania.
“Napenda sana mambo ya urembo, Yaani ususi na make up”
hapo baba yangu alibabe majukumu na kumsomesha MELANIA kwenye chuo kikubwa sana cha urembo na ususi hapa jijini.
Miaka ilikimbia na baada ya miaka mwili Mimi nikiwa naanza chuo mwaka wangu wa kwanza, Melania alikuwa ameshamaliza elimu yake ya urembo na alikuwa yupo Nyumbani akisubilia baba amfungulie saloon.
Ndani ya mwaka huo huo mama MELANIA aliweza kupoteza maisha na kumuacha MELANIA akiwa yatima.
Baba yangu hakutaka kabisa kumuacha Melania na akamchukua kabisa na kumfanya ni familia Rasmi na sio Mtoto wa KIJAKAZI Kama ilivyokuwa mwanzo.
********
Ouk jamani tuachane na yaliyopita na tuendelee uku mbele.
KWa sasa mimi bado ni Mwanafunzi wa chuo na Nipo nachukua masters.
KWa upande wa Melania ni tayali Ana saloon yake mjini na tayali anajulikana kiasi na anapiga pesa kwa Namna moja au nyingine.
Kitu ambacho kipo kwangu ni kwamba sijawai kumpenda huyu Binti ata kidogo, Maombi yangu ya kila siku ni kwamba huyu Binti aondoke Nyumbani kwetu tu na akaishi mbali.
Ukiniuliza sababu ya kumchukua MELANIA ni kWa sababu tu sio ndugu yetu lakini pia ni Mtoto wa kijakazi na nilikuwa naona Kama anatumia tu pesa za familia yangu ikiwa hausiki.
KWa upande wa dada yangu ambaye alijulikana Kama Diana, yeye alikuwa tayali ni mfanyakazi kwenye kampuni ya baba yetu, lakini pia Diana alikuwa akimpenda sana MELANIA.
Chuki yangu kWa Mela nilifanya kWa Siri sana Tena sana ata hakuna mtu alikuwa anaweza kujua.
Ikiwa ni siku ya kazi kaama kawaida, wazazi na dada Diana wote walienda kwenye majukumu na Nyumbani tulibaki Mimi, mela na Mdada wa kazi tu.
Siku hiyo mela hakuwa ameenda kazini kwake kwani alidai Kuwa anaumwa tumbo.
Baada ya kuona Kuwa Nyumbani tupo wenyewe, Nilizunguka nyuma ya Nyumba na kwenda kwenye Nyumba ambayo alikuwa akikaa mela.
Nilifika na pasi na kupiga hodi niliingua na kumkuta akiwa amejilaza kitandani uku akiangalia mambo yake ya urembo kwenye mtandao.
“Kenzo, mbona ili suala la wewe kuingia chumbani kwangu pasi na kupiga hodi unaona ni la kawaida sana ??”
Mela aliniuliza.
“Kwamba ? Yaani kwenye Nyumba ya baba yangu pia unataka Nipige hodi, halafu ni Kama unajisahaulisha Kuwa Mimi ni Nani kwenye huu mjengo si ndio ??”
Nilimuuliza uku nikibinua sura yake kwa kutumia kidevu chake.
“Aaah unaniumiza Bwana “
Mela alinifokea.
Kitendo cha mela kunifokea kilinikela sana na kujikuta nikimchapa kibao Kimoja cha mashavu hapo mela Akatulia na kuniangalia tu.
“Usije ukatumia huu mdomo wako kunipandishia sauti ata siku moja nitakuja nikichakaze sura yako hiyo”
Nilimwambia.
Muda huo huo Niliinuka na kuvua t-shirt yangu na kutupia pembeni mela akazungumza.
“Siko vizuri Leo “
“Hauko vizuri ukiwa Unamaanisha nini ? Ebu jiandae hapo nipige show zangu niende chuo”
Kitu ambacho amkijui ni kwamba, uwa namtumia mela kimwili muda wowote na Saa yoyote ile ninayoitaka mimi.
Mchezo huu umeanza tangu pale tu mama yake alivyofariki, kwani ndio muda ambao mela alianza kuishi Mwenyewe kwenye hii Nyumba yetu ya nyuma.
Sikuwai kujali chochote kuhusu yeye, sikujali Kuwa yuko period au laaah nilichojali ni Mimi kupata mambo yangu.
Kabla hatujaanza chochote kile, simu yangu iliita na Demu wangu ninayempenda sana ndio alikuwa akipiga haraka nikapokea.
“Yes babe….”
“Babe nimewai chuoni kwaajili yako lakini cha ajabu ni kwamba Ujafika mpaka muda huu”
Alizungumza mpenzi wangu na sauti yake ya kudeka.
“Niko njiani Babe, soon nafika kuna jam kidogo”
Nilimaliza kuzungumza na my wangu kisha nikamgeukia mela na kumwambia.
“Jiandae kwaajili ya usiku, hakikisha Kuwa haufungi mlango “
“Sawa “
Alijibu mela.
Naweza nikasema Kuwa hiyo ndio ilikuwa pona ya mela kwa wakati huo lakini isingekuwa simu Basi ningekuwa Napiga vyangu tu.
ITAENDELEA…
MELANIA (najutia kukupoteza)
MTUNZI: PATRICIA DAMAS
SEHEMU YA: 02
www.tupohapa.com
SONGA NAYO……
🤍🤎🤍🤎🤎🤍🤎🤍
Niliingia chumbani kwangu chap nikajiandaa na kuondoka zangu chuoni, nilifika na kukuta mpenzi wangu akiwa ameniletea chakula kutoka nyumbaani kwao.
Sawa Kenzo Mimi Nina wapenzi wengi lakini huyu msichana ambaye anajulikana kama Rachel nampenda kuliko kitu chochote, Yaani ndio msichana ambaye ata akiniita saa 8 za usiku nitaamka na kwenda kumuona.
Majila ya Jioni nilishika njia na kurudi nyumbaani, nilifika Nyumbani kWa kuchelewa sana kutokana na foleni kubwa sana.
Nilifika na kukuta familia nzima ikiwa mezani ikipata chakula lakini Mela hakuwepo.
“Umewai Bwana anzia mezani Kijana wangu “
Baba aliniambia baada ya kuniona, kWa utulivu nikasogea na kuuliza.
“Melania yuko wapi jamani ??”
Kila mtu akanigeukia na kuniangalia kisha wakacheka na kusema.
“Yaani wewe na Mela, Yaani yeye pia alivyokuja kuchukua chakula alikuulizia “
Nilitabasamu tu na kujibu.
“Kwahiyo ameenda kula chumbani kwake au ? Kwani anaumwa sana ??”
Niliuliza nikionesha wasiwasi mkubwa sana juu yaMela.
“Ameitaji utulivu tu, lakini pia muache anaonekana Kuwa hayuko Sawa “
“Sawa “
Nilijibu kWa unyonge na kukaa kwenye meza ya chakula na kuendelea kupata chakula.
Nilikula uku nikiangalia kiti cha mela, Yaani Mimi kwa ndugu na wazazi wangu nilionesha kumjali sana mela, Yaani nilionesha kila aina ya upendo ambapo haikuwa rahisi wao kugundua Kuwa kuna mambo mabaya namfanyia mela.
“Halafu kesho ni siku yake ya kuzaliwa mjue “
Niliwaambia.
Hapo kila mtu ndio alikumbuka ni wazi Kuwa walikuwa wameshasahau.
“I want to make her happy so nitamfanyia surprise ya family party, nitafurahi Kama mtaungana na Mimi katika kumpatia mela Furaha “
Nilizungumza utazani Namaanisha vile kumbe Nina langu moyoni.
Baada ya kumaliza kula kila mtu akaingia chumbani kwake na Mimi nikaingia chumbani kwangu.
Nikachukua simu yangu na kumpigia simu mela lakini hakipokea ata simu yangu moja, Nilimchukia sana Walahi.
Kitu ambacho amkijui ni kwamba, Mimi sijawai kuchati na Mela, mara zote uwa nampigia tu. wasiwasi wangu ni kwamba kuna siku mela anaweza akatumia chatting Kuwaonesha wazazi ukweli wa mambo yote.
Sikukoma kumpigia simu nilipiga simu zaidi ya Mara 10 lakini hakupokea kabisa.
Muda huo huo dada Yangu Diana akaingia chumbani.
“Mbona kama hauko sawa. ??”
Dada yangu aliniuliza.
“Aaah, niko Sawa “
“Mmmh unasemaje uko Sawa na Nakuona kabisa Kuwa hauko Sawa, nambie kaka Angu handsome shida ni nini “
Alizungumza dada yangu uku akinishika kwenye bega.
“Melania Apokei simu zangu 🥹”
Nilizungumza uku nikitamani kulia.
Kuhusu kulia Bwana nilikuwa natamani kulia kweli 😂🙌 Yaani muda huo upwiru ulikuwa umekaba koo halafu wa kunisaidia ndio Apokei simu.
“Ahaaha, khaaah Mdogo wangu punguza sasa jamani, Yaani unampenda mela mpaka unashindwa kujizuia, Mela amekupa nini ??”’
“Kunipa nini ukiwa Unamaanisha nini ??”
Nilijibu uku nikifuta mchozi ambao tayali umeshanidondoka.
“Na unalia jamani, eeeh ngoja nimpigie mimi “
KWa upande wa dada yangu aliamini Kuwa Mimi nampenda Mela kimapenzi na alifanya kila juhudi kuhakikisha Kuwa mela anakuwa WiFi yake wa halali.
Dada Diana alimpigia simu mela na hakuchukua muda akapokea.
“Mela umelala ??”
Diana alimuuliza mela.
“Hapana sijalala kuna shida “”
Mela aliuliza.
“Shida ipo Tena kubwa sana, kaka yangu anakupigia simu upokei mpaka analia uku “
Alizungumza dada yangu na kuangua kicheko cha hali ya juu akinicheka mimi 😂🙌.
“Nilikuwa nikisali ndio maana sikuweza kupokea, Mwambie niko Sawa Ila kWa sasa nalala tutaonana kesho”
“Aaaah jamani Ebu ongea nae apate amani kaka yangu “
Basi hapo nilichukua simu na kuongea na Mela, Tulizungumza kwa Furaha Sanaa na mwisho tukaagana na dada yangu akarudi chumbani kwake.
********
Siku ziliendelea kwenda uku nikizidi kumtesa mela pasi na kujali maumivu yake.
KWa upande wa mela Bwana alinipenda kindaki Ndaki, Yaani ukiachana na visa vyote ninavyomfanyia mela lakini yeye ni ananipenda kuliko kawaida, ananipenda mpaka ajielewi huyu msichana.
Ikiwa ni siku ya weekend, na ni siku ambayo nilikuwa na birthday party ya Rafiki yangu, niliweza kuwaaga wazazi na kweli wakanipatia ruhusa lakini baba akazungumza.
“Umchukue na Mela uwende nae kidogo akapate kuinjoy “
Aaaah Walahi nilichukia sana, Yaani ni siku yangu ya kuinjoy halafu naanza kuambiwa nibebe watu niende nao, bora ata angekuwa mtu mwingine lakini mi huyu Binti ambaye simpendi ata kidogo.
“Hapana baba me sitaenda kokote “
Mela Alijibu kwani pia na yenye alikuwepo kWa Wakati huo.
“Mela Binti yangu, wewe umekuwa ukijifungia tu Ndani kwako, Yaani wewe maisha yako ni saloon Nyumbani, Nyumbani saloon, aaaah Mara moja moja uwe unatengeneza marafiki wapya sio Kila siku unakwama na huyu Kenzo ooooh 😂🙌 utakosa wachumba wa maana”
Alizuungumza mama yangu na akaingizia utani wake.
Katika watu ambao wanatamani mimi nimuoe mela Leo kesho ni mama yangu na dada yangu Diana.
Yaani umu Ndani kwetu mela anaonekana Kama mailaaika hivi, kiufupi mela anapendwa sana kutokana na tabia zake njema.
Mela alijitaidi sana kukataa lakini mwisho wa siku alishindwa na safari ikawa ni Mimi na mela.
“Hakikisha unamlinda mwenzio na mnarudi wote”
Alizungumza mama wakati huo Mimi na Mela ndio tulikuwa tunaondoka.
Walahi mela alipendeza sana Tena sana, kWa jinsi ambavyo mela alipendeza ata Mimi sikuacha kum tazama na mwisho nikamwambia.
“Umependeza sana Leo “
Mela alifurahi sana akakatabasamu na kubaki akiminyaminya vidole vyake, hii feeling anayoipata mela kwa wakati huo wanaweza kuelewa watu ambao wame fall in love tu, kama ambavyo mela ananipenda Mimi.
Hatimaye tulifika eneo husika, lakini kabla hatujashuka kwenye gari, nilishangaa sana kuona alama ambayo ilikaa kama moja chini ya bega la mela, kWa shauku nikagusa na kumuuliza.
“Ni nini hii??”
“Sio kitu”
Mela Alijibu na kutaka kushuka lakini nilimvuta na kukishika kWa nguvu na Mela akaonesha kuumia.
“NI nini hii “
Nilimuuliza kWa hasira sana, akili yangu iliwaza labda ni mambo ya uchawi maana huyu Binti simuamini ata kidogo.
“Ni njia ya kuzuia kupata mimba Inaitwa kijiti”
Alijibu mela kWa hasira uku akiangalia pembeni .
“Kumbe ndio maana, unajua kila siku najiuliza au Ninashida siwezi kuzalisha kumbe wewe umeweka huu ujinga wako hapa “
“Ujinga gani sasa ? Kujilinda ndio ujinga ? Kenzo wewe ujawai kujali siku za hatari Wala siku zozote zile Itakuwaje nikishika mimba Mimi 🥹”
Alijibu uku akitaka kulia.
“Hayo machozi yako siyataki kabisa, iko hivi kesho nisikione mwilini mwako”
“Lak….”
Kabla hajamaliza kuzungumza nikafungua mlango wa gari na kushuka .
JE MELA ATATOA KIJITI ? NA VIPI KAMA ASIPOTOA KENZO ATAMFANYA NINI ?
MELANIA (najutia kukupoteza)
MTUNZI: PATRICIA DAMAS
SEHEMU YA: 03
www.tupohapa.com
SONGA NAYO……
🤍🤎🤍🤎🤎🤍🤎🤍
Nilishuka na kuanza kuingia Ndani, lakini muda huo Mela alikuwa amekaa tu Ndani ya gari akinishangaa ninavyondoka.
Baada ya mwendo mfupi niliamua kurudi nyuma nikasimamma kwenye Kioo na kumuuliza.
“Hautashuka au ??”
Mela akaniangalia kwa muda kisha kWa sauti ya kilio akajibu.
“Nitakuwa Sawa Kama nitabaki hapa just go “
Aaah kwakuwa ata Mimi nilikuwa sitaki kuongozana nae niliona ni Sawa tu, niliingia Ndani na kuendelea kuinjoy na Rafiki zangu, kulikuwa na mziki mnene, pombe za kutosha, chakula cake na kila kitu, ilikuwa ni party 🎉 Fulani hivi ya kishua sana.
Baada ya kama Lisa Kimoja hivi, Mela aliingia Ndani lakini hakuwa Mwenyewe, alikuwa na mshikaji wangu ambaye alijulikana Kama kenned na wengi tulikuwa tukimuita Kenny, muda huo Kenny alikuwa ameshikilia mkono wa Mela na akimuongoza kwenye sehemu ya vinywaji.
Sijui ni nini kilitokea lakini nilijikuta niliumia sana, nilijikuta nikipata hasira ya haraka baada ya kuona Kuwa Mela yupo na mwanaume mwingine na amemshika na mkono kabisa.
“Unakunywaga pombe ??”
Kenny alimuuliza Mela.
“Aaaaaah hapana jamani, juice inanitosha sana”
Alijibu Mela uku akitabasamu.
Walahi hii ilizidi kunikela zaidi, nilitamani kuwafuata lakini nikatulia kwani muda huo nilikuwa nimekaa na kipenzi changu Rachel.
Basi Mela akachukua juice na chakula kisha yeye na Kenny wakaenda kukaa kwenye meza ambayo walikuwa ni wao tu hakukuwa na watu wengine.
“Wanajuana au ??”
Nilimuuliza kimoyomoyo uku nikiwaangalia.
“Babe, Mbona kama hauko hapa unawaza nini ??”
Rachel aliniuliza baada ya kuona Kuwa Nimekuwa na mood tofauti kabisa na ile ambayo nilikuwa nayo mwanzo.
“Noooh babe, nilikuwa naangalia wale wanavyocheza, unaitaji tucheze au ?”
Nilimuuliza ili tu kuvukuga mada.
“Hapana kwakweli, nimechoka sana na naona hii pombe imeshaanza kufanya kazi miguuni “
Basi tuliendelea kupata moja moto moja baridi na kusikiliza mziki mizuri kutoka kwa DJ wetu.
Majila ya sana 6 Rachel aliniaga na kuondoka, hapo na Mimi haraka haraka nikasogea kwenye meza ambayo alikuwa amekaa Mela na Kenny, Walahi walikuwa wakipiga story na kucheka Kama ni watu ambao wnaafahamiana kitambo sana.
“Time to go “
Nilimwambia mela.
Kenny aligeuka na kuniangalia kisha akauliza.
“Broh Mbona unataka kuondoka mapema jamani eeeh ? Ata hivyo njoo Nilitaka nikutambulishe Rafiki yangu Mpya “
Alizungumza Kenny pasi na kujua Kuwa Mimi namjua Mela kuliko yeye anavyomjua.
“She’s Mela, na ni kijakazi wa Nyumbani kwetu for years “
Nilijibu kwa dharau ya hali ya juu.
Hapo Kenny alibaki akiniangalia kisha akamuangalia Mela na kumuuliza.
“Kumbe mnajuana ? “
“Yaaah ni Mtoto wa mwisho wa boss wangu na yeye ndiye mtu ambaye Nimekuja nae Leo, Kenny ilikuwa wakati mzuri sana na wewe Naomba nikuage Rafiki yangu “
Basi Mela na Kenny wakaagana kWa kumkumbatia, hii nayo iliniuma Walahi lakini sikutaka kuonesha.
Nilimshika mkono Mela na moja kwa moja tukaingia kwenye gari.
“Umemjuaje kenny? “
Nilimuuliza kwa hasira sana.
“Ni Rafiki yangu “
Alijibu Mela kWa kifupi sana uku akichezea simu yake.
“Nikiwa mazungumza na wewe please iko kisiimu chako weka mbali kabisa, halafu niambie, Kenny Rafiki yako kivipi umemjulia wapi ??”
“Aaaah Mbona Kama unanishautia ? Kwani sitakiwi kujuana na watu au ? Kenny ni mmoja kati ya wateja wangu pale saloon Mara nyingi uwa anawalea watoto wa dada yake kuja kusuka pale saloon kwangu “
Daaaah hii iliniuma, kwahiyo hawa ni watu ambao wanajuana sana na wanazungumza Yaani tuseme ata kuwasiliana uwawanawasiliana sana tu.
“Namba zake unazo ? “
Nilimuuliza.
“Yeye kama Mteja wangu lazima niwe na Namba yake, muda mwingi uwa ananitumia mitindo ya watoto ikitokea Kama watoto wanakuja na Dereva tu “
“Futa Namba yake “
Nilijikuta nikilopoka.
“Unanionea Wivu au ? Hivi kwanza kipindi iki ndio ungefurahi kwamba yupo mtu ambaye tayali nimemzoea, ilibidi uniweke Karibu kabisa na huyo mtu ikiwezekana anipende na anichukue mazima nitoke kwenye maisha yako “
Daaah huyu Mela kukaa na Kenny masaa kadhaa tu tayali ameanza kunijibu Kama hivi.
Nilipata hasira sana, pasi na kufikilia nikajikuta nikianza kumpiga Mela.
Mwanamke ni mwanamke jamani, mela hakuweza kurudisha ata Ngumi moja Kwangu, alibaki akilia tu na kuomba masada, kitu kibaya ni kwamba, ata Msaada hakuweza kupata kwani mziki wa Ndani ulikuwa mkubwa sana na hakuna mtu ambaye angeweza kumsaidia.
Baada ya kumpiga sana niliwasha gari na kWa pamoja tukaondoka Nyumbani.
********
Siku iliyofuata, ni siku ya Jumapili na ni siku ambayo sisi kama familia uwa tunaenda kanisani pamoja, kila mtu aliamka asubuhi na kujiandaa na makutano yetu uwa Ni kwenye packing ya magari.
“Wewe umepatwa na nini ??”
Mama yangu alimuuliza Mela
Kwa mshangao wa hali ya juu baada ya kumuona akiwa amevimba sana usoni na jicho lake moja likiwa limeziba.
Mela alishindwa kujibu zaidi aliniangalia Mimi.
Kwakweli nilimpiga Sawa lakini sikutalajia Kuwa atakuwa Namna hii Yaani kiufupi nilimuharibu usoni.
“Umepatwa na nini jamani ??”
Baba alimuuliza na kumsogelea.
Kabla mela ajajibu na kuniharibia nikazungumza.
“Jana amepigana na msichana mwenzie ambaye walikuwa wanashare mwanaume mmoja “
Hapo Mela alishtuka sana Walahi akuamini Kuwa naweza nikatoa uongo mkubwa kiasi iko, uongo ambao ungemuharibia sifa nzuri ambayo aliijenga pale Nyumbani.
“What ? A man ? “
Mama yangu aliuliza kwa mshangao sana, Yaani mule Ndani kwetu Sijui watu uwa wanafikiliaga Kuwa Mela ni bikra Sijui ni malaika, maana walishtuka sana baada ya mimi kudanganya.
“No mama, Kenzo amenipiga Jana”
Weeeh Mela si ndio akaamua kuvunja ukimya na kulopoka, hapo kila mtu akanigeukia Mimi.
Nyieeeh uwa sinaga Kigugumizi lakini nilipata cha gafla.
“Aaa, aaah,daddy li……”
Kabla sijamaliza jamani baba yangu alinishushia kibao Kimoja cha mkono wa mwanaume kwenye shavu langu.
“Daddy, ujanisikiliza lakini “
Nilianza kujitetea, baba yangu jamani hakuwai kunipiga labda uko utotoni lakini Leo ameamua kunipiga kwakuwa tu Melania amemwambia Kuwa Mimi nimempiga.
“Ndio Melania nimempiga lakini mnajua sababu ni nini ? Mimi nitawambia, Melania amekuwa akitoloka Nyumbani usiku na na kwenda uko nje kwaajili ya kujiuza, na Jana ndio nilijua baada ya yeye kugonganisha wanaume zake wawili ambao ni wateja zake katika hiyo kazi yake chafu anayoifanya, Melania hiyo saloon ni kivuli cha kuficha uchafu wake, baba kila mtu anajua Kama Melania anaishi na sisi na Jana Jina lako limechafuka Saana kwaajili ya huyu Binti, baba uwezi amini, Mela anamahusiano na Rafiki yangu Kenny “
Muda huo huo simu ya Melania iliita na Kenny ndio alikuwa akipiga.
“Pokea “
Nilimwambia.
Basi baba akampokonya simu Melania na kupokea kisha akaweka loudspeaker.
“Hello Melania, me nimeshafika kanisani kwenu Nimekuja kusali uku kwaajili yako”
Weeeh nyie mie ni kitukuu cha mtume, imagine nimedanganya halafu msaada umekuja chap, Yaani Kenny pasi na kujua akanisaidia 😂🙌.
Baba kwa hasira akapiga simu ya Melania chini na kufanya ingawanyike kisha aka…..
ITAENDELEA…….
MELANIA (najutia kukupoteza)
MTUNZI: PATRICIA DAMAS
SEHEMU YA: 04
www.tupohapa.com
SONGA NAYO……
🤍🤎🤍🤎🤎🤍🤎🤍
KWa hasira baba akazungumza .
“Ndani wote “
Eeeeh baba akiwa kwenye hali kama hiyo hakuna kuuliza maswali kinachofuata ni sote kufuata tulichoambiwa.
KWa upande wa Mela alibaki akilia tu, alichuchumaa chini na kuanza kuokota simu yake, hii simu Bwana nakumbuka ilikuwa ni zawadi kutoa kwa baba, Yaani baba ndio alimnunulia Mela hii simu.
Baada ya kumaliza kuokota moja kWa moja akaja Ndani, ile kuingia tu baba akauliza.
“Hizi habari azijazagaa uko mitandaoni ??”
KWa haraka nikajibu.
“Hapana baba, niliweza kızibiti kila kitu na mpaka asubuhi hii nimeweza kuangalia kila kitu kiko Sawa”
Nilijibu kwa kujiamini kwani najua kabisa Kuwa Nilizungumza uongo.
“Mela Kama hiki kitu ni kweli Walahi Binti yangu umejua kunivua nguo, ukatazwi Kuwa na mahusiano, wewe ni Mtoto wa kike utaolewa Leo kesho , na ili kuolewa lazima uanzie kwenye mahusiano, lakini ili la wewe kujiuza limeniumiza sana, ni kitu gani unakosa umu Ndani ? Kuna siku umewai kuomba ruhusa ya kutoka Tukakukatalia ??”
Alizungumza baba yangu kwa utulivu wa hali ya juu.
“Mela nakupenda sana Binti yangu Tena sana, Kiukweli umeniumiza sana moyo wangu, mimi kama baba yako nimeumia sana, Nimekuwa nikifunga na kusali kwajili yenu ninyi nyote, wewe na Diana sijaacha kuwaombe wema wa maisha yenu lakini wewe unataka kuyaharibu maisha yako “
Daaaah baba yangu Alizungumza Kwa uchungu sana, Yaani baba yangu aliamua Kuwa baba kabisa kwenye maisha ya Melania na hapo alikuwa akiumia sana baada ya kusikia taarifa za hovyo sana juu ya Binti yake mrembo.
Baba aliongea Mengi sana siku hiyo na safari ya kwenda kanisani ikafa.
“Diana mpeleke huyu hospital na urudi nae “
Baba Alimwambia dada Diana ampeleke Mela hospital kwaajili ya Yale majeraha aliyoyapata kwajili ya kipondo nilichompatia.
“Hapana baba nimeshakanda nitakuwa Sawa. “
“Mela Alizungumza kWa sauti ya chini sana”
“Kukanda sio dawa lazima Wakaangalie usalama wa jicho lako, na wewe Kenzo mwanzo mwisho Leo kunyanyua mkono wako na kumpiga mela au yeyote Yule Sawa ??”
“Sawa baba “
Nilijibu uku nikiangalia chini.
*******
Siku ziliendelea kwenda na kila mtu aliendelea kuamini Kuwa Mela alikuwa Akijiuza.
KWa upande wangu sikuacha kula utamu wa mela, Yaani sio kwamba nilikuwa nikimuitaji sana hapana ni vile tu ni process zangu za kumkosesha amani pale Nyumbani.
Nilifanya utaratibu wa kumtoa mela kile kijiti chake ili tu niweze kujua Kama Nina uwezo wa kuzalisha au laaah, sio kwamba nilikuwa sina wanawake wengine, lakini mela ndiye mwanamke Pekee ambaye nilikuwa nikimmudu Yaani ni shwaaaaah.
Maisha yaliendelea kwenda na mela akaendelea na shughuli zake za saloon.
Urafiki wa mela na Kenny ulizidi kuota mizizi, ikafika kipindi mpaka Kenny akamnunulia Mela simu lakini Mela akakataa kWa kuofia Nyumbani atasema nini.
Mela aliendelea tu kutumia kisimu chake cha batani cha elfu 25 ambacho mwanzo alikuwaga anatumiaga mama yake mzazi.
Ikiwa ni Majila ya usiku, Kama kawaida, nikachomoka chumbani kwangu Na kwenda chumbani kwa mela kwaajili ya mambo yangu.
“Hivi mela ujawai kushika unauzito kabisa tangu umetoa ile kinga ??”
Nilimuuliza uku nikirudiShia mavazi yangu mwilini.
“Kwani unataka Mtoto ??”
Mela aliniuliza uku akiwa Amenikazia sana macho.
“Nataka kujua tu kama Nina uwezo wa kuzalisha au laaah”
“Kwamba Mimi ni chombo cha majaribio au ? Hayo majaribio yako kafanye kWa Rachel, mwanamke ambaye ata akibeba mimba Una uwezo wa wewe kusimama Kama mume na baba wa Mtoto “
Kwanza nilishangaa sana hizi habari za Rachel huyu amejuaje, Sawa Melania anajua Kama Nina mahusiano lakini sikuwai kumwambia Kuwa mwanamke wangu anaitwa Rachel.
“Mmeanza Kunikalia Vikao wewe na Kenny ??”
Nilimuuliza.
“Kwani utaki watu wajue kuhusu mahusiano yako na Rachel au ? kwanza toka nje “
Daaah Ila mela jamani amekuwa ni mwanamke Mwenye hasira sana Sasa hivi, Yaani aniogopi ata kidogo na ananijibu hivyo muda na Saa yoyote ile anavyojisikia yeye.
KWa hasira nikatoka nje na kuondoka zangu.
Siku iliyofuata baada ya kutoka chuoni, nilifunga safari na kwenda kazini kWa Mela, Sijui ni kitu gani kilinipeleka lakini siku hiyo nilijikuta nilitamani sana kwenda kwenye saloon ya mela.
Nilifika na kukuta wadada kadhaa ambao walikuwa wameweka foleni kwaajili ya huduma.
“Karibu “
Mela alinikaribisha kWa bashasha sana.
Ila Mimi na mela Bwana, mbele za watu ni Kama ni watu ambao tunapendana sana lakini ukija Nyumba ya pazia uwiiiiih ni chuo na paka.
Siku hiyo Nilimsubili mpaka alipomaliza na kWa pamoja tukarudi Nyumbani.
*******
Miezi mitatu ilipita uku maisha yakisonga mbele.
Tukiwa kwenye meza ya chakula, mela hakuwa akila kabisa alibaki akichezea chakula na kijiko chake pasi na kupeleka mdomoni.
Muda huo huo mela aliinuka na mbio mbio akatoka nje kwaajili ya kwenda kutapika, Walahi hii ilinistua sana na Mimi ndio nikawa wa kwnza kuinuka na kwenda kumuangalia.
“Shida nini ??”
Nilimuuliza.
Mela aliniangalia tu na kuendelea kutapika.
“Mela Kama unamimba usije ukanitaja please “
Nilimwambia.
Muda huo huo sauti ya mama ikasikika.
“Kama atakutaka utamfanya nini ??”
Nika……
UWIIIIIIH SIJUI NATOKAJE LEO JAMANI….NAKUJA
MELANIA (najutia kukupoteza)
MTUNZI: PATRICIA DAMAS
SEHEMU YA: 05
www.tupohapa.com
SONGA NAYO……
🤍🤎🤍🤎🤎🤍🤎🤍
Nilishtuka sana Walahi, moyo wangu ulipata wasiwasi wa gafla, kuna muda nilitamani ata Ardhi ipasuke nipate kutumbukia Walahi, Yaani Leo ni Kama naenda kuumbuka hivi mbele ya familia yangu.
“Akikutaja utamfanya nini ??”
Mama aliniuliza Tena na alikuwa yupo serious sana, nyieeeeh niliogopa kuliko kawaida, nirudi nyuma maana Nilihisi Kama ananisogelen sana hivi.
Basi Mela akamaliza kutapika mama akamshika na kuanza kuingia nae Ndani.
“We nyauba njoo Ndani “
Khaaaah Leo hii mama ananiita Majina ambayo ata sikuwai kuyasikia kwenye maisha yangu jamani 🥹😂🙌, ukisikia za mwizi ni 40 Basi ndio hizi jamani ila zangu ni Mbona kama zimewai kufika.
“Karibu Tunapata mgeni Mpya kwenye familia “
Mama Alizungumza baada tu ya kufika kwenye meza ya chakula, haraka nikadakia.
“Lakini mama Una Uhakika gani Kuwa Mela ni mjamzito ? Labda huo uyoga ndio umemchefua maana ata hivyo hauna Radha nzuri Leo “
Mama aliniangalia kisha akatabasamu na kumuangalia mela kisha akaamuuliza.
“Unasiku ngapi tangu ujigundue Kuwa wewe ni mjamzito ? Mela usinidanganye maana niliingia chumbani kwako na nilikuta kipimo Chako na ninacho mimi mpaka Leo “
Nyie macho yalinitoka sana, Yaani nilikuwa nikitetemeka utazani sio Mimi ambaye uwa namvimbishia kufua mela wa watu.
“Ni mwezi mmoja na week Mbili mama”
“Kwahiyo Mela Binti yangu umeamua kuanza kuitwa mama kabla ya kuitwa mke ??”
Baba alimuuliza Mela.
“Wakati unamuuliza Mela, muulize, na Kenzo aliyeamua kuanza kuitwa baba kabla ya kuitwa Mume “
Hapo Sasa ndio akili ya baba yangu ikachangamka na kugundua Kuwa Mimi ndio muhusika mkuu wa ujauzito wa Mela.
“Baba sio Mimi, Mimi Sijui labda Kenny “
Nilianza kujitetea lakini Mela akazungumza.
“Sikuwai Kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Kenny ata siku moja, sikuwai kushiriki tendo na mwanaume mwingine yeyote Yule zaidi ya Kenzo katika maisha yangu, najua inakuwa ni ngumu kuniamini kutokana na habari mlizozipokea hapa katikati lakini, ukweli ni kwamba, Kenzo alinipiga kwaajili ya Wivu wa mapenzi tu, Kenzo alinipigia kwakuwa alichukizwa na urafiki wangu na Kenny “
Uwiiiiiiih Leo Mela ameamua kunichoma jamani Sijui Kama natoboa Leo 💔🥹.
Sehemu hiyo Bwana kuna A/C nzuri kabisa lakini nilijikuta nikianza kuswet mpaka jasho likalowanisha T-shirt niliyokuwa nimeivaa.
Baba kWa hasira akanyanyuka na kunisogelea na kuniuliza.
“Are you responsible for this??”
Weeeeeh Sijui ata ububu nilitoka wapi lakini kWa wakati huo nilikuwa ni zaidi ya bubu 😂🙌 Sijui mnanielewa lakini, Yaani Ububu ulikuwa ni pro Max 😆 ujanja kwisha kabisa ata nguvu ya kujitetea sina mwisho nikazungumza kWa sauti ya upole sana.
“Am sorry baba “
Daaaah hapo ni Kama ndio nilikubali kila kitu nilichomfanyia Mela, Yaani nilijikuta nikikubali Maneno yote aliyozungumza mela.
“Kwahiyo Mimi najua ni mapenzi ya dada na kala kumbe mnanizunguka si ndio ? Haya mambo ya kununuliana zawadi, kujaliana na kila kitu haikuwa ni kwaajili ya dada na kaka si ndio ??”
Yaani baba yangu hakuwa tayali kabisa kwajili ya Mimi na Mela Kuwa pamoja.
“Am sorry baba”
Nilijibu uku nikianza kulia ili kupunguza makali ya hii kesi inayoendelea.
“You will take a responsibility as a man, As a father to be, na next week tutaandikisha ndoa kanisani huyu Mtoto atazaliwa Ndani ya ndoa “
Alizungumza baba na kwa hasira sana akaondoka chumbani kwake.
Eeeeeh ukisikia shimo ulilochimba umeingia Mwenyewe ndio hii sasa, Mwenyewe nilitaka kufanya kizazi cha Mela Kuwa majaribio lakini jaribio limetiki na limeamua kuja na cheti kabisa 😂🙌 ukisikia chururu si ndo ndo ndo ndio hii sasa.
“Ariririiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii”
Mama yangu Alipiga vigelegele uku akinipepea na mtandao wake ni wazi Kuwa alifurahishwa sana na habari ya Mimi kumuoa Melaa.
“Hatimaye Mungu ameamua kuwaunganisha mapema sana “
Alizungumza dada yangu ambaye alikuwa akisubilia kWa hamu sana kumuita Mela Wifi.
KWa upande wangu nilichukia sana na haraka nikakimbilia chumbani.
“Haiwezi kutokea Mimi kuoa Mtoto wa Kijakaazi “
Nilizungumza kimoyomoyo uku nikizunguka uku na uku pasi na kupumzika.
“Nikimuoa Mela ni wazi Kuwa Rachel ataniacha “
Niliendele kujiongelesha Walahi nyie uchizi uwa aupigi hodi Yaani unakuwa muda wowote ule.
Majila ya Saa 8 usiku, niliamka na kuanza kuweka nguo zangu kwenye begi kwaajili ya kutoloka, muda huo nilishapanga kwenda mbali sana ili tu kumkwepa mela.
Nilimaliza kupanda nguo nikajiandaa kisha huyo nikaondoka zangu, kwa muda huo hakukuwa na mtu wa kunizuia kwani kila mtu alikuwa amelala.
Safari yangu kwa usiku huo niliamua kufikia hotelini ili niweze kupumzika na kujua kitu kinachofuata ni kipi.
Bwana Bwana, nikiwa kwenye process za kuchukua Chumba, mambo ndipo yaliponichanganya, hapo ndioo nilipogundua Kuwa account yangu ya bank ilikuwa imeefungiwa ili nisiweze kutoa pesa.
“Shiiiiiiit “
Nililalaama uku nikipiga mguu juu “
“Kuna shida kaka ?”
Mdada wa mapokezi aliniuliza.
“Haikuhusu na wewe “
Nilimjibu na kuondoka zangu, Walahi baba aliniweza Sijui ata wazo la kufungia account alitoa wapi na Sijui alikuwa amewaza nini mpaka akafanya kitu Kama iko.
Sasa bila pesa Bwana hakuna sehemu nitaenda Walahi.
Usiku huo huo nilifunga safari na kurudi Tena Nyumbani na nilifika Majila ya Saa 11 kasoro alfajrii.
“Welcome back son “
Alizungumza baba yangu ambaye alikuwa amekaa sebuleni kwenye giza Totoro”
“Am sorry daddy “
“Kenzo hizi am sorry utazizungumza sana tu Kama Hautajubali makosa yako na kukubali Kuwa mwanaume, Ebu washa taa ili tuweze kuonana”
Nilisogea na kwenda kuwasha taa kisha nikaenda kukaa alipokuwa amekaa baba.
“Ulikuwa na plan gani na maisha ya Mela ??”
Baba aliniuliza.
Walahi swali la baba ni dogo sana lakini lina maana kubwa sana, Yaani ni swali ambalo linaitaji umakini wa hali ya juu.
Nilitulia kidogo kisha nikajiabu.
“Baba, sikuwai Kuwa na lengo baya juu ya Mela, najua nimekosea kwakuwa ulitulea sisi kwakuwa dada na kaka, lakini muda wote imekuwa ni ndoto yangu ya Mimi Kuwa mume halali wa Mela, 🥹 baba ukweli ni kwamba nampenda sana mela Tena sana , lakini tamaa zangu za mwili zinakatisha mipango yangu, nilitamani kumuoa mela muda ambao tayali nitakuwa nimeajiliwa lakini naona ndoto yangu umezima kama mshumaa. Naenda Kuwa mume katika umri Kama huu lakini pia bab ambaye sijajipanga “
Nyieeeeh niliongea kwa kulia kabisa utazani nilikuwa nikimaanisha vile.
Baba yangu alinielewa kWa asilimia 100.
“Mistake lazima ziwepo aswa kwenye huu umri wenu watoto wangu, Mimi Kama baba yenu nitakuwa na ninyi, Kenzo be a man okay kila kitu kitakuwa Sawa “
Nilimaliza kuzungumza na. Baba kisha nikarudi chumbani kwangu nikiwa na hasira ya Mbogo.
*********
Miezi mitatu iliisha na hatimaye nikawa mume halali wa Mela Yaani baba yangu alihakikisha Kuwa Mtoto wangu na mela anazaliwa sisi tukiwa Ndani ya ndoa.
Siku ya ndoa yetu, mimi na Mela, wazazi wetu walituzawadia Nyumba pamoja na gari.
Kuanzia siku hiyo mimi na mela tukaama Nyumbani na kwenda kwenye makazi yetu mapya.
“Mela andaa chakula kizuri sana Rachel anakuja Leo “
Nilimwambia mela.
My zangu iko hivi, Sawa nilikuwa Nimemuoa mela lakini Mimi na Rachel penzi letu lilibaki pale pale.
“Yaani Mimi niingie jikoni nimpigie mke mwenzangu ?”
Mela aliniuliza uku akiangaika kukaa chini na tumbo lake kama kichuguu cha Siafu.
“Mke mwenzio ni Nani ? Mela acha kumfananisha Rachel na vitu vya ajabu kwenye maisha yangu Nipo na Rachel tu sio wewe “
Hapo vurugu likaanza na ulikuwa ni ugomvi wa kutosha.
Mimi na Mela kugombana ni kawaida sana na Nyumbani kwetu ni uwanja wa vita.
Mela alinyanyuka na kutaka kuondoka lakini nilimsukuma kWa nguvu sana na kupelekea yeye kugonga tumbo lake kwenye meza.
“Mela, mela…”
Nilimuita mela mfululizo uku nikimtikisa..
KWa wakati huo damu zilianza kumiminika kutoka chini lakini pia na puani mwake.
Mela alikuwa akiugulia maumivu tu na baada ya muda akatulia kabisa hakuwa akitikisika Wala nini.
Nilijaribu kusikiliza mapigo yake ya moyo lakini hayakusiikika ata kidogo, nilijaribu kuangalia Mshipa wake wa kwenye mkono Kama unadunda lakini hakukuwa ata na dalili, niliweka mkono wangu puani mwake ili kuhisi hewa ya mpuuzi yake lakini pia kukawa ni ola ola…..
JE MELANIA NI MZIMA AU LAAAAH ??
SOMA MAELEKEZO
Bonyeza hi "Soma Kitabu" kisha itakupeleka kwenye fomu yaku login, hakikisha ume login na namba uliyojiunga nayo ndipo utaendelea sasa kusoma kitabu chote