Mpaka na mimi nikawa Azmm Tv burudani kwa wote kwaajili ya tabia za kwanamke wa uswahilini niliyemuoa. Mwanamke anamdomo jamani sijawai ona. Anaongea kama chiriku na maneno yake sasa yalivyo na shombo. Hakuona hasara kunitukana hata mimi mume wake. Uswahili wa huko mtaani aliuleta mpaka ndani ya nyumba. Mwanamke hajui nini maana ya mdoa, hajui kumuheshimu mumewe wala kumtii. Nikajua hata kwanini nilimuoa alafu kumuacha nashindwa sielewi nianzie wapi. Yote kwa yote kitandani Mke wangu Aziza mjanja sana. Naona alinilogea hapo. Kitandani mtoto wa kike anajituma balaaa atakupeleka mpaka nchi ya ahadiπππ. Akinipa mautamu namsamehe maudhi yake yote na kuyasahau kabisaππππ.
Siku moja tulitibuana na mke wangu Aziza si akaniambia nakibamia na sijawai mfikisha hata kileleni basi hapo ndipo aliyatimba nikasema naanza kugawa mtarimbo wangu yaani AZMM TV BURUDANI KWA WOTE. Nilianza na hao hao mashova zake waliokuwa wananichukulia pouwa, nikasema kwa kupitia uwanaume wangu wataniheshimu. Nilihakikisha nawachanganya kama kachumbali ili wawe na heshima. Basi kila niliyepiga nae show aliniganda kweli kweli na kunimwagia sifa kibao walimuona Aziza mshamba anaichezea bahati. Wengine walikuwa tayari kuachana na wanaume zao ili niwaoe mimi.......USIKUBALI IKUPITE HII STORY. NI TAMU MPAKA TAMU TENA....
SIMULIZI : TATIZO KAMDOMO
MTUNZI : NURU HALISI
SEHEMU 01
MWANZO.....
Tulimaliza kupanga vitu ndani ya chumba chetu mimi na mke wangu Aziza baada ya kuamia makazi mapya. Baada ya kila kitu kuwa sawa tulienda kuoga, chumba kilikuwa Self, choo cha ndani.
Tulipanda kitandani kwaajili ya kuupumzisha mwili ndipo niliibua naongezi mawili matatu.
"Wife!".
"Niambie my habity".
"Naomba ubadilike kitabia na hii iwe nyumba yetu ya kupanga ya mwisho, tukitoka hapa twende kwenye mji wetu. Kuhama hama nyumba za kupanga kila mala napo sio sifa bali ujinga".
"Lakini mume wangu wewe ndo sio muelewa tu. Na hujui namna ya kuishi na watu vizuri".
"Naelewa ila kila kitu kwenye maisha kina mipaka na unatakiwa kufanya kwa kiasi. Huu ni wakati wetu mimi na wewe kuanza familia. Naomba muda mwingi uutumie na mimi mke wangu. Nakupenda sana na unaelewa hilo. Kukuacha siwezi ila naomba upunguze uswahili. Wewe ni mke wa mtu uwe na mipaka kwenye nyumba yako".
"Baba nimekuelewa tusije fika mbali sasa. Sitaki zogo". Tulikumbatiana na kilichofuata hapo vilio vya maha.....ba tu.
Palikucha asubuhi, siku ilianza upya tukiwa kwenye mazingira mapya. Nyumba tuliyopamba ilikuwa nyumba kubwa na mwenye nyumba na familia yake walikuwa wanakaa hapo hapo. Sisi tulipanga chumba cha uwani kilijitenga na nyumba kubwa.
Mke wangu Aziza aliniandalia chai na baada ya hapo aliniandaa kwenda kazini huku nikimsisitiza sitaki mazoea na watu maana kinachotufanya tuhame nyumba hizo nyengine ni hao hao watu.
Nilijipa matumaini kuwa mke wangu amebadilika baada ya wiki nzima kupita bila kuona dalili zake za uswahili ndani ya nyumba. Nikienda kazini namuacha mwenyewe ndani na nikiludu namkuta mwenyewe. Siku hiyo nilitoka kazini mapema nilipitia kwenye duka la nguo nilimnulia mke wangu gauni zuri la stara.
Nilifika nyumbani majira ya saa 11 jioni. Nilishangaa baada ya kukuta viatu vya watu wengi sio chini ya wanne mlangoni.
"Mmmmh!. Kumekucha". Niliyasema hayo kwa sauti ya chini. Huko ndani Aziza alisikia harufu ya manukato yangu alijua moja kwa moja nakaribia kufika au nimefika.
"Hadhry ameludi. Jamani naombeni mtoke ndani kwangu mume wangu anaingia muda si mrefu.
"Mmmh!, umejuaje na wewe kama ameludi na tupo wote ndani?" Jirani mmoja alimuuliza. Akijisemea moyoni au Aziza mchawi.
"Nasikia harufu ya pafyu yake hebu inukeni muende jamani".
"Unatukata stimu ujue. Tuondokeni jamani". Jirani mwengine aliongea hayo. Waliinuka sitaki nataka walifungua mlango walikutana na mimi nimesimama pembeni ya mlango, walijua moja kwa moja nilikuwa nawasubilia wao watoke ndani.
Niliingia ndani nilimkuta Aziza anapanga vitu maana vilikuwa shagala bagala. Nilienda kujilaza kitandani.
"Leo mapema mume wangu?". Aziza aliniongelesha wala sikumjibu. Alijua nimechukia basi alichukua ule mfuko nilioludi nao alitoa ile nguo alifurahi sana alinishukuru huku ananipiga mabusu mengi mengi mpaka nililegea.
Aiseee mie kwa Aziza sikuwa na ujanja, licha ya mapungufu yake ila kwenye Tendo yupo vizuri ni mjanja sana. Basi baada ya kumaliza mchezo niliongea na mke wangu kwa utaratibu kuwa sitaki mazoea na majirani ya kuingizana mpaka ndani. Ndani kwenyewe tuna chumba tu bola ingekuwa chumba na sebule.
"Mume wangu nimekuelewa ila tatizo mie siwezi kumfukuza mtu jamani. Wananifuata wenyewe. Nitaonekana najisikia na na roho mbaya kwasababu hatuna njaa, wanasema ndani kwangu kuzuri panavutia, pananukia wanatamani kukaa muda wote". Mke wangu alikuwa anaongea kama mjinga. Ni kweli maisha yetu ya kawaida tu ila ndani kwangu kuna vitu vingi vya thamani na tumevipanga kwa mpangilio vimeleta muonekano mzuri ndani".
"Lakini si unajua mwanamke mpumbavu huivunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe?".
"Aaaah! Wee baba usinitishe bhana. Kwanza tuachane na hayo, unaonaje leo ukanipumzisha kupika mume wangu, unitoe hata diner jamani maana muda mrefu kweli hatujatoka" nilimkubalia japo sikuwa na ratiba ya kutoka.
Siku zilizidi kusonga mbele, kuishi na mwanamke mswahili kama wewe sio mswahili kazi sana aiseee. Sherehe kila kukicha hela zinaishia huko kwenye kutunzana kutaka sifa. Maendeleo nyumbani mpaka afanye mwanaume.
Siku moja nililudi nyumbani kutoka kazini kama kawaida niliwakuta majirani na wapangaji wenzangu ndani, ilibidi niishie nje kibalazani. Basi nilitulia zangu pale balazana napigwa na mbu kama wote, wao huko ndani hawana habari kabisa tena vicheko vimetawala. Basi nikawa najiuliza mwenyewe nimeoa mwanamke au kituko.
Basi nikiwa nimekaa pale balazani kuna mdada jirani alikuja.
"Vipi kaka?".
"Freshi niambie?".
"Nimekuona umekaa mwenyewe hapa muda mrefu sana".
"Yeah napunga upepo".
"Mmmh! Sio kweli, ngoja kwanza nakuja". Aliondoka muda mchache aliludi akiwa na Hotpot la chakula". Akaanza kuniongelesha kwamba nisimfikilie vibaya ila amenihurumia tu nimekaa nje muda mrefu na hao waliopo ndani hawana hata dalili ya kutoka.
"Kwani wewe ni nani kwanza. Yaani sikujui hunijui unanipa chakula nile kivipi yani?".
"Wewe kula tu na uwe na amani siwezi kukudhuru kwa chochote". Yule dada alinibembeleza sana nile. Nikaona isiwe kesi na kweli njaa ilikuwa inauma. Nilianza kula ulikiwa wali nyama, chakula kilikuwa kitamu mpaka nilijikuta namsifia mpishi bila kutarajia........ITAENDELEA........
SIMULIZI :TATIZO KAMDOMO
MTUNZI : NURU HALISI
SEHEMU 02
ENDELEA......
Chakula kilikuwa kitamu nilijikuta namsifia mpishi bila kutarajia.
"Aiseee chakula kitamu sana. Unajua kupika, bila shaka utakuwa umesomea jiko vizuri kabisa na kama hujasomea basi kungwi wako anastahili tuzo". Nilijikita nambwagia sifa yule binti, ma mpaka muda huo sikujua anaitwa na anaishi wapi.
"Hahahahaaaa! Taratibu jamani huko ndani wasije wakatusikia ikawa balaa. Kula haraka niondoke na vyombo vyangu".
"Unaitwa nani kwanza. Alafu chakula kitamu huwezi kukifanyia pupa, unatakiwa ule taratibu huku unaisikilizia radha nzuri ya chakula.
"Una maneno wewe".
"Aya niambie unaitwa nani?".
"Naitwa Hinna".
"Unajina zuri sana".
"Naitwa Hadhry. Asante kwa kujali".
"Usijali kaka. Mie nakaa hapo nyumba ya pili. Nilikuja hapa nashida na mama Asha yupo humu ndani kwako basi baada ya kukuona hapa nimekuhurumia. Sijui kwanini wanawake wengine hawajitambui. Yaani wanaipata bahati wanaichezea. Wengine tunatafuta ndoa kwa hudi na uvumba hatupati jamani".
"Hujaolewa?".
"Bado na nimekata tamaa napambana na maisha tu".
"Usikate tamaa MUNGU atakupa tu mwanaume wako. Siku zote unaambia hakuna kitu kizuri kama majira. Majira ikifika kila kitu kinakuwa sasa hakuna atakayeweza kuzuia majira ya MUNGU kwaajili yako".
"Ni kweli kabisa". Tuliendelea kupiga story mbili tatu huku mie nakula chakula kitamu kutoka kwa Hinna". Basi huyo Hinna ni binti mzuri tu. Ana sura nzuri na umbo zuri tu ila kwa sura hamzidi mke wangu Aziza.
Nilimaliza kula Hinna alibeba vyombo vyake huyo akaondoka. Mpaka saa nne usibu bado nilikua nje. Hawa wa ndani hawatoki. Niliona mke wangu siku hiyo ameniamulia kweli kweli.
"Aiseeee unataka nife kwa kuliwa na mbu wee mwanamke?". Nilimtumia ujumbe mke wangu.
"Uweeee! Nyie odokeni haraka, mume wangu kumbe kaludi analiwa na mbu huko" basi alivyokuwa anawatimua wenzie nilisikia vizuri.
"Lakini imefika patamu. Subili basi si inakalibia kuisha na wewe". Mama Asha mpangaji mwenzetu aliongea hayo.
"Weee huna akili eeeeh!, kwaiyo mume wangu aendelee kuliwa na mbu eti mpaka iishe. Ebu tokeni tokeni bhana".
"Basi ngoja tuone mzee kikala kama atazinduka. Yaani baba amekula hasara huyu watoto sijui sita ila kama kazaa wawili tu loooh!" Majirani badala ya kutoka ndani wakaanza kuongea kuhusu kombolole tena.
"Jamani kuweni wastarabu basi tusije kuonana wabaya". Walitoka nje walinikuta nimejilaza pale kibalazani.
"Aaah! Shemeji kumbe umeludi?".
"Za asubuhi". Mama asha ni mdada wa makako tu alinisalimia za Asubuhi.
"Saivi ni usiku na wewe ebu toka hapa". Mama Tesha alimshushua. Basi mie nilikuwa nawaangalia tu wanavyojiongelesha. Hata baada wa wapangaji wenzangu kutoka ndani kwangu mimi niliendelea kujilaza pale kibalazani na vile nilikuwa nimeshiba wali na sijoto la nyama basi ndo sikuwa na habari.
"Mume wangu bhana. Yaani kumbe umeludi muda mrefu tu umekaa nje".
"Sasa ndani ningekaa wapi. Wenzio wanagala gala mpaka kitandani. Unakumbuka nilikwambia kuwa hii ndo nyumba yangu ya mwisho kupanga, si unakumbuka?". Nilimuuliza Aziza.
"Nakumbuka baba na hata mie sitokubali kuhama hama".
"Basi usijali nitavumilia yote labda ushindwe wewe". Niliyasema hayo na baada ya hapo niliingia ndani nilimuacha Aziza amesimama pale pale kibalazani.
"Mmmh!, makubwa haya".
Aliingia ndani alinikuta nipo bafuni naoga, basi nilitoka bafuni kinapanda kutandani.
"Mume wangu chakula tayari. Tujumuike wote basi my husband".
"Mimi nishakula wewe endelea tu. Leo nimechoka sana nahitaji kupumzika kwa amani kabisa". Niliyasema hayo na baada ya hapo nilivuta shuka nikajifunika gubi gubi.
"Makubwa haya leo. Eti kupumzika kwa Amani. Kwaiyo umenisusia na kula eti si ndiyo?, kama ulikuwa unajua huli utakula huko huko si ungeniambia tu kuliko kunichosha". Basi Aziza aliongea weee ila hata sikumjibu. Wanaume hatuongeagi sana ni maneno mawili matatu tunanyamaza". Basi Aziza aliongea weee mie kimya tu.
Palikucha asubuhi aliamka ameninunia. Anakawaida asubuhi ananiandaa kwenda kazini ila siku hiyo aliamka na kuwa busy na kazi za nyumbani hata chai hakuniandalia. Na mie sikumsemesha nilijiandaa kwenyewe baada ya kuwa tayari niliweka pesa ya matumizi mizani nikaondoka kuelekea kazini.
Siku hiyo kazi hazikwenda kabisa. Napenda amani ndani ya nyumba muda wote na zaidi Aziza alijua kuukamata moyo wangu. Licha ya mapungufu ila upendo wangu kwake ulikuwa pale pale.
"Broo shida nini?". Rafiki yangu aitwae Erasto aliniuliza.
"Wanawake kuna muda wanatuchanganya akili sana".
"Kwanini tena. Shem amekufanyaje?".
"Yaani sijui niseme ana utoto mwingi au uswahili umezidi. Nampenda sana mke wangu ila tabia zake zinanikatisha tamaa kabisa.
"Pole. Badae baada ya kutoka kazini tutaongea zaidi. Ni kweli kila ndoa zina changamoto zake ila kuna changamoto nyengine hazivumiliki ndo maana unaambiwa kabda ya kuoa hakikisha unayemuoa ataweza kuvumilia mapungufu yako na wewe uvumilie yake.
"Hilo ni kweli kabisa". Basi tulikubaliana baadae tutaongea zaidi.
Upande wa nyumbani mke wangu alitoka alienda kusalimia mashoshti zake. Basi huko akakutana na mambo ya shughuli.
"Mwenzenu mie mke wa mtu natakiwa kupunguza hizi heka heka, mume wangu atanichoka mjue?".
"Na wewe sijui uliharakishia nini ndoa. Yaani juna hata miaka 30 una haraka na ndoa. Hujamaliza kula bata la ujana unakimbilia ndoa ndo madhara yake hayo. Siwema aliongea hayo.
"Kheeeee!. Miaka 27 mnaina bidogo
Kheeeeee!, wallah. Bola nimestilika maana Umri unaenda".
"Shoga bado unalipa alafu wee mzuri bhana. Una uwezo wa kuwa na mwanaume yeyote umtakae nashangaa umemkimbilia mwanaume kwangu pakavu, wewe sio wa kuishi stoo. unalala na majiko chumbani". Amina rafiki yake mwengine aliongea hayo.
"Mnanikela sasa. Kwaiyo nimekosea kuja kuwasalimia. Mambo yangu ya ndoa na maisha yangu ya ndoa niachieni mwenyewe. Haya niambieni hiyo shughuli lini na mambo yanayotakiwa nijipange mapema, kuhusu umasikini wangu niachieni mwenyewe. Bola nimestilika kuliko ningebaki kuwa madunga embe kama nyie". Aziza aliyasema hayo basi ukaibuka ugomvi mkubwa, wenzie walichukia kwanini kawaita madunga embeπ€£π€£π€£......NAKUJA.......
SIMULIZI : TATIZO KAMDOMO
MTUNZI : NURU HALISI
SEHEMU 03
ENDELEA.......
Hapakuwa na maelewano tena baada ya kukwidana nguo na kuchaniana. Aziza aliludi nyumbani sio vile alivyoenda. Mimi baada ya kutoka kazini tuliongozana na rafiki yangu Erasto mpaka kwenye moja ya bar. Tuliagiza vinjwaji(sikuwa mnywaji wa pombe).
Vinywaji vililetwa mimi nililetewa soda na maji huku mwenzangu aliletewa bia. Basi tulianza kunywa huku story za hapa na pale zinaendelea.
"Unajua bwana mdogo. Katika safari ya mafanikio inahitajika utulivu na amani ya moyo".
"Kweli kabisa". Erasto aliniuliza nina shida gani kwenye ndoa yangu. Ni rafiki yangu wa muda mrefu ila sikuwai kumfungukia matatizo yangu. Siku hiyo niliufungua moyo wangu nilimueleza namna tunavyoishi na mke wangu".
"Aiseee pole sana".
"Usinipe pole maana haitonisaidia kitu. Nahitaji ushauri kutoka kwako nifanyanye ili mke wangu aishi kwenye sheria zangu".
"Tatizo naweza nikakushauri alafu ukaniona mbaya ndo maana waswahili wanasema. Usiingilie ugomvi wa watu walioonana undani wao au wanandoa".
"Wewe nishauri, usijali. Mpaka nakuambia ujue nimechoka japo bado nampenda. Sitegemei kama utaniambia nimpe taraka".
"Ishi nae vile anavyotaka usimwambie tena usimuonyeshe maumivu yako wala machukizo kwa mambo anayoyafanya. Pendelea kuwa mkimya muda mwingi, punguza kumuonyesha kuwa unamuhitaji sana kwenye maisha yako na la mwisho kuanzia sasa ongeza kasi kwenye kujiwekea akiba ili utimize malengo, si unajua ndugu yangu kuna maisha baada ya leo".
"Ni kweli kabisa. Ntafanyia kazi ushauri wako".
"Vipi biashara yako inaendaje?".
"Biashara inaenda ila ninahitaji kuchukua mkopo nifungue ofisi kubwa".
"Mkopo wa bei gani?".
"Milioni 20, sema nakwama sina kutu cha dhamani kwaajili ya dhamana na nimekosa mdhamini pia".
"Sikia nipe wiki moja nilishughulikie hilo ila usiniangushe". Basi Erasto alijitolea kunikopesha pesa kiasi cha shilingi milion 20 nitakuwa namludishia taratibu.Mwenzangu maisha safi hana njaa kabisa ana biashara nyingi tu hapa mjini na mke wake ni mjasiriamali mzuri sana.
Nililudi nyumbani nilimkuta Aziza amenuna balaa na siku hiyo palikuwa swali hakuna watu ndani. Nilimsalimia ila hakuitikia basi na mie sikujali. Niliingia bafuni kuoga na baada ya hapo nilipanda kitandani nikawa busy na simu yangu. Nilimuona Aziza ametoka nje, kwa mbali nilisikia anaongea na simu ila sikujua anaongea na nani.
Basi baada ya kama nusu saa hivi mama yangu mzazi alinipigia simu.
"Kuna nini kinaendelea huko?". Mama aliniuliza hata kabda ya salama.
"Mama ni vizuri kujuliana hali kwanza. Unaendeleaje huko nyumbani?".
"Huku wazima, umemfanyaje mwenzio amenipigia simu usiku huu anaongea huku analia?"
"Haaaaa! Mama, mbona tupo sawa tu". Licha ya mapungufu ya mke wangu na tabia zake mbaya ila sikuwai kumshtakia popote. Mtu wa kwanza kumwambia tabia za mke wangu ni Erasto rafiki yangu. Mimi sio mwanaume wa kumsemea mke wangu kwa watu vibaya hata kama ana ubaya.
Ukimya wangu ndio ulisababisha mke wangu kuonekana mzuri kwa wazazi wangu na ndugu zangu. Ana sifa ya ucheshi na heshima kwa familia yangu. Basi mama yangu ulikuwa anampenda mno.
Sikuwa na lakujitetea maana sikujua Aziza amemwambia nini mama na mimi sikutaka kumwambia mama makosa ya mke wangu.
"Ishi na mtoto wa watu vizuri. Nasikia umeanza uhuni huko hata kula nyumbani huli. Hadhry ukitaka kufanikiwa haraka ishi na mkeo vizuri".
"Mama nimekuelewa".
"Haya malizaneni, nachotaka kusikia amani kutoka kwenu".
"Sawa mama". Kwa heshima ya mama yangu nilitoka nje kumfuata Aziza. Nilimkuta amekaa balazani analia.
"Wife!". Nilimuita ila hakuitikia aliendelea kulia, nilimsogelea karibu nikakaa kando yake.
"I'm sorry mke wangu".
"Unanitesa kwasababu unajua nakupenda siwezi kukuacha Hadhry?". Nilijishusha kumuomba msamaha Aziza japo yeye ndo mwenye makosa.
Tuliingia ndani Aziza alipakua chakula tulianza kula wote, furaha ililejea ndani.
"Mke wangu napenda kila siku tuwe hivi. Napenda amani sana sema hujui tu". Niliongea hayo.
"Basi mume wangu tule kwanza sio vizuri kuongea wakati wa kula". Nilimuangalia tu Aziza nikatabasamu.
"Alafu mume wangu bola nimekumbuka".
"Si tumalize kula kwanza alafu tuongee. Sio vizuri mke wangu kuongea wakati wa kula".
"Nitasahau bhana".
"Haya niambia".
"Kuna shughuli ya shoga angu". Baada ya Aziza kusema hayo tu nikajua kumekucha. Hapo nitapigwa mizinga ya hela na nikimnyia atafanya anavyojua yeye na amani ndani ya nyumba itatoweka............Kuishi na mwanamke mswahili yahitaji moyo mgumu kweli kweli..........ITAENDELEA..........
SIMULIZI : TATIZO KAMDOMO
MTUNZI : NURU HALISI
SEHEMU 04
ENDELEA.......
Basi Aziza alisema kiasi gani anachohitaji kwaajili ya shughuli. Hapo anaongea huku ananilisha, Wallah niliona kama kile chakula kinanikaba kooni kwa hasira nilizokuwa nazo. Hapo moyoni nawaza, hivi huyu mwanamke atabadilika lini?, hakuna siku tunakaa tunaongelea kuhusu maendeleo ya maisha yetu. Na hata tukiongea basi ni mimi ndiye najiongelesha.
Hakuwa na Akili ya maendeleo yeye anawaza tu shughuli za watu, kuvaa, saloon kila wiki, kubadilisha viatu. Yaani asisikie viatu vipya vya Zara vimetoka basi hiyo kesho atavitaka.
Hapo ashaniambia anahitaji laki moja tu kwaajili ya shughuli. Na alivyokuwa anaitamka sasa ni kama vile elfu moja. Anakwambia nataka laki moja tu mume wangu, yaani laki moja tu kwaajili ya shughuli nyengine ya zawadi na vitu vidogo vidogo nitajibana nyumbani nitapata.
"Sawa". Nilimjibu tu kwa mkato, Aziza aliguna alijua kabisa sijapenda.
"Inatosha wife nimeshiba. Nilisitisha kula maana chakula chenyewe niliona kimepotea radha. Yaani unakuta mwezi mmoja shughuli mbili na zote ananiomba hela. Maisha yenyewe hayajatukalia sawa. Nikakumbuka na maneno ya Erasto muda mchache aliniambia niishi nae kwenye sheria zangu na nisimame kama mwanaume ndani ya nyumba na sio kuishi kwenye sheria za mwanamke.
Hapo kichwani nilikuwa nawaza yangu huyu nimuanzie wapi na hiyo laki moja safari hii simpi hata mia. Mida hiyo ilikiwa saa 3 usiku.
"Aziza!"sauti ilisikika kutoka nje ya mlango wetu. Mke wangu alimkaribisha kwa kumwambia aingie. Nilimkata jicho la machukizo ila Aziza hakujali kabisa.
Muda huo mie nilikuwa nimilaza mitandani naperuza mitandaoni huku nikiwa nimevalia boxes juu nipo kifua wazi. Nilimshangaa mke wangu anamwambia mtu aingie ndani na mie nipo nusu utupu. Ilibidi nivute shuka haraka nikajifunika. Mlango ulifunguliwa yule mtu aliingia ndani.
"Eeeeh shoga kulikoni usiku huu majumbani kwa watu?". Aziza alimuuliza chausiku.
"Mwenzangu acha tu. Kwanza imeisha?".
"Nini?".
"Kombolela, maana naona matangazo hapo". Kabda Aziza hajamjibu matangazo yaliisha muendelezo wa kombolea huo!.
"Nikajua imeisha. Nakwambia nimekaa ndani kwangu mapigo ya moyo yapo juu juu wee bola nipitwe na vyote ila sio kombolela shoga. Eeeeeh kumbe shem shem yupo. Shem mambo!". Chau ni mwanamke malika ya mke wangu ana hana mume ila nae ndo kama Aziza tu uswahili na mdomo sasa"
"Salama tu". Nikamjibu kwa kujilazimisha ila chau hata halujali ndo kwanza alikaa na chini akawa anaangalia tamthiria. Aziza mke wangu alikuwa anaguna tu. Mala mama Asha nae huyo amefika, basi wakaanza kuongezeka mpama watoto wa mama mwenye nyumba wakike wawili.
Uvumilivu ulinishinda kabisa nilijikuta natoka zangu nje na shuka langu kiunoni. Basi baada ya mimi kutoka nje ndo nikawapa nafasi wengine waliosimama wakaenda kukaa na kitandani. Yaani hiyo nyumba ilikuwa too much sasa bola zote nilizowai kupanga hapo palizidi. Huko kwengine nilipopita walikuwa wanatawala kama mimi sipo nikiwepo hawaji au nikiludi wanatoka wenyewe bila kuambiwa sasa hapo uwepo usiwepo vyote sawa.
Nilikaa pale kibarazana kama nusu saa mke wangu alitoka nje alinikuta nimejilaza balazani.
"Mume wangu". Aliniita kwa sauti ndogo.
"Hivi Aziza haya maisha mpaka lini eeeeh!. Kwanini huniheshimu?".
"Sio hivyo mume wangu ila tatizo hawa wote hawana Azam Tv wengine vifurushi vimeisha, nashindwa kuwafukuza wataniona na roho mbaya".
"Basi sawa. Nenda kakae nao muangalie hiyo kombolela ila dawa inachemka unakumbuka nilikwambia nini?, nakuacha ufanye unavyotaka ila tu usiniulize chochote kunihusu".
"Punguza jazba jamani my love".
"Sawa weee wala usijali. Mie nipo sawa ila nakwambia tu ukweli". Huko ndani shangwe likalipuka kama lote mpaka mimi na Aziza tuliokuwa nje tulishtuka kuna nini tena. Aziza aliinuka haraka akakimbilia ndani. Mimi roho ya yangu kwenye vitu vyangu tu wasije kuniharibia. Basi na mke wangu nae alivyoingia ndani hakutoka.
Nikaendelea kuliwa na mbu pale kibalazani. Mala paa! Namuona Hinna anapita , nilimkumbuka vizuri maana mtu aliyekutendea wema huwezi kumsahau. Baada ya dakika chache akapita tena akiwa amebeba chupa ya maji uhai ndipo nikasema kumbe alienda dukani.
Basi ile ananigeukia tu kidume nikampungia mkono kumpa hai. Hinna alinipungia nae mkono hakuishia hapo alinisogelea mpaka karibu na mimi.
"Mambo kaka!".
"Safi mzima".
"Niko pw, naona na leo unapunga upepo". Aliongea huku anatazama mlangoni kwangu kulivyojazana viatu vya majirani.
"Upepo watu, napigika tu hapa".
"Pole ndo ukubwa huo. Ila nakuhurumia ujue. Watu wa mtaa huku ukiwazoea nao wanakuzoea vibaya. Sasa utakaa hapa mpaka saa ngapi jamani na kulivyo na mbu si uwafukuze?".
"Hapana siwezi".
"Basi twende kwangu ukalale".
"Naanzaje, mke wangu mkorofi vibaya mno".
"Ni wasiwasi wako tu. Mie nafanya kukustili kwa muda na usinichukulie vibaya. Unapoenda kwangu mie nitajumuika nao hao ndani kwako wakitoka na mie natoka nakuja kukustua unaludi kwako" basi nilimuona Hinna ni mwanamke wa kipekee aisee, na nilivyokuwa nimechoka nilikubali, basi akanipeleka mpaka kwake kwa kuibia ibia watu wasituone. Tuliingia chumbani aiseeeee.........ITAENDELEA.......
SIMULIZI : TATIZO KAMDOMO
MTUNZI : NURU HALISI
SEHEMU 05
ENDELEA........
Hinna alinipeleka mpaka nyumbani kwake, tuliingia ndani ya chumba chake aisee nilishangaa. Ndani kwake alijipanga vyema. Swali la kwanza nililomuuliza.
"Umeolewa?".
"Jamani Kaka Hadhry. Sina mume sina mchumba kiufupi nipo single napambana na life".
"Aiseee kama kweli hongera".
"Amini na uwe huru navyokuacha lala tena fofofo kabisa hakuna wa kukufanyia fujo humu".
"Sawa". Hinna alitoka chumbani na moja kwa moja alienda kwangu. Hakuwai kuwa na mazoea na mke wangu zaidi ya salamu basi alienda kwa gia ya kumuulizia mama Asha.
Mie nilipanda kitandani kwa Hinna hapo kichwa kimejaa mawazo tele hata usingizi sijui ulinipitia saa ngapi.
Waliendelea kuangalia TV mpaka saa sita za usiku hakuna tamthilia waliyoiacha iwapite basi na kwakuwa mke wangu anapenda umbea ndo kabisa. Wengine wanaangalia TV wengine wanapiga umbea. Aziza hata alipotoka nje hakunikuta na wala hakustuka kabisa.
"Tuondokeni jamani na sisi tuna waume zetu. Mida ya kuhudumia ndoa hii". Chausiku aliongea hayo.
"Weee nae muda wa kuhudumia ndoa au kuwanga saivi wewe kama unawai kwenye harakati zako za usiku nenda tu. Mie mume wangu hata hayupo na akiludi kalewa bwiiii! Anajitupa kitandani kama mzoga". Mama Asha aliongea hayo ilibidi Aziza aingilie kati maana ungefuata ugomvi.
"Heeeee! Jamani makelele na maugomvi ndani kwangu sitaki. Hapa peace and love kwanza muda umeenda saivi saa saba kasoro hii. Kila mtu aende kwakwe". Aziza aliongea hayo.
Walianza kutoka mmoja mmoja Hinna alianza kuzuga kuongea na mama Asha alitaka ashuhudie wote wametoka ndipo aje kuniamsha niende kwangu.
Alipohakikisha wametoka wote alikuja kwake alinikuta nimepitiwa na usingizi sina hili wala lile, alinitazama kwa dakika chache huku akiwa amekaa kando yangu.
"Mkaka mzuri ila anateseka na mapenzi tena sio mapenzi ndoa. Ila sijawai kuona mwanamke asiyejielewa kama Aziza looooh!". Hinna aliyasema hayo alitamani hata nafasi ya Aziza ingekuwa yake ila upande mwengine alijisemea mimi si mwanaume wa ndoto zake.
Hinna aliniamsha kwa kunitingisha mgongo. Niliamka nikiwa najinyoosha. Yaani nilijikuta nimesahau kama nipo kwa watu na sio kwangu.
"Au utalala hapa mpaka asubuhi. Yaani ajabu mkeo hata habari hana kabisa. Hivi kaka Hadhry ilikuake mpaka ulimuoa Aziza hukupata muda wa kumsoma tabia?". Hinna aliniuliza akionekana kusikitishwa na nayopitia kwenye ndoa yangu.
"Tuachane na hayo Hinna. Tambua tu kila ndoa na changamoto yake".
"Ila yako naona kiboko sijawai kuona. Aya nenda nyumbani kwako washaondoa wote".
"Asante kwa kujali".
"Usijali. Karibu tena". Niliondoka nikaludi kwangu nilimkuta Aziza ameshafunga mlango na taa za ndani zilizimwa kuashiria amelala.
"Aziza!". Nilimuita mke wangu mala moja tu aliitikia.
"Kalale ulipoenda si unaona unanikomoa. Kwa taarifa yako hunikomoi babu wewe, nikianza kuyafanya machafu yangu mbona dunia itatikisika, jifanye mjanja tu". Mke wangu alianza kubwata akiwa ndani. Nilihisi huenda amejua nilikuwa kwa Hinna. Basi nilianza kumuomba msamaha pale pale mlangoni.
Muda wa karibu lisaa lizima nilikuwa mlangoni nambembeleza Aziza anifungulie mlango. Sikuwa na namna zaidi ya kumbembeleza mke wangu. Nilitoka ndani na boxes tu pamoja na shuka nililojifunga kiunoni ningeenda wapi na hiyo boxes usiku huo.
Aziza alifungua mlango mie nilikuwa hoi aiseee hapo nimembembeleza weee mpaka basi. Nimechambuliwa kama majani ya maboga. Nilipoingia tu ndani nilipata kitamdani nikajifunika shuka gubi gubi kuepusha shari. Aziza aliendelea kubwata. Yaani Kamdomo kamdomo πππ.
Basi aliongea mwenyewe mpaka alivyochoka mie sikumjibu. Alipanda kitandani kila mmoja alilala na makasiriko yake.
Palikucha asubuhi aliamka amenuna balaa!. Nilijiandaa kwenyewe nikamuachia pesa ya matumizi nikaenda kazini.
Siku hiyo nilifunga ofisi yangu mapema nililudi nyumbani kuitafuta amani na mke wangu. Aziza sijui alinipa nini maana licha ya tabia zake ila sikuwai kuwaza kumuacha wala kunyanyua mkono kumuadhibu.
Nilifika nyumbani ajabu Aziza alinipokea vizuri na zaidi aliniomba msamaha basi nilijikuta nasahau yote na kumtazama mke wangu kwa upya. Ile laki moja aliyoniomba kwaajili ya shughuli nilimpa baada ya kumaliza mechi kitandani πππ.
Mke wangu aliingia jikoni mimi nikawa nimekaa kitandani nachezea loptop yangu. Mala simu yangu ilianza kuita mpigaji alikuwa Erasto.
"Upo wapi mwanangu nimepita ofisini mwako nimekukosa".
"Anhaa! Leo nimefunga mapema broo kuna mambo home hayakuwa sawa si unajua tena".
"Anhaaa nilipita hapo kwaajili ya ile ishu na mzigo nilikuwa nao" alivyoniambia hivyo nilijua anamaanisha nini, mbele ya hela mbona nilichangamka. Nilimuomba Erasto tuonane kama ana nafasi nyengine tena. Sikutaka siku ipite.
Nilianza kujiandaa Aziza aliniuliza naenda wapi nilimwambia kuna ishu ya biashara nafuatilia.
Tulionana na Erasto maeneo ya karibu na mitaa niliyokuwa nakaa. Kwwakuwa alikuwa na usafiri wake aliniambia ananifuata yeye na kweli tulikutana kwenye moja ya bar Iliyo barabarani . Tuliagiza vinywaji na nyama choma tulianza kula taratibu huku tunapiga story za naendeleo.
Erasto aliniambia ananipa hela ila atahakikisha nasimama kiuchumi kwaiyo kila kitu ataniongoza na zaidi aliniambia nisimwambie mke wangu kuhusu hizo pesa.
Alinikabidhi kiasi cha shilingi milioni 20 kwenye bahasha ya kaki, Tukiwa tunaendelea kula huku tunapiga story kwa mbali nilimuona Hinna anapita na alikuwa anakuja usawa wa bar akiwa amevalia sketi ndefu nyeusi, viatu vya kudumbukiza simpo, shati mikono mirefu la blue bahari amejifunga ushungi mweusi kicheani, huku kwapani ameibana pochi yake. Nilimuangalia sana mpaka Erasto alinistukia.
"Huwezi amini jana nimelala kwa huyu dada bila kupenda". Nilijikuta naongea hayo .
"Ilikuaje, mbona hana muonekano mbaya kusema anajiuza?".
"Yaani acha tu". Hinna nae aliniona pale bar basi nilimpungia mkono nilimuita. Alikuja tulisalimiana pale baada ya salamu Erasto alimuomba akae.
"Agizia unachotaka". Hinna alikuwa na wasiwasi ndipo nilimuondoa hofu. Aliagizia chips mishkaki na maji ya baridi.
"Anaonekana ni binti mzuri sana na hana mambo mengi. Wanawake wa hivi sio wakuchezea ni wakuwekwa ndani". Erasto aliongea hayo Hinna mwenyewe alikuwa anaona aibu.
Gafla bin vuu! Aziza huyo kafika hapo , cha kwanza aliibinua ile meza ya chakula na vinywaji, vyote vilivyokuwepo mezani pamoja na simu vilisambaratika............ITAENDELEA......
SOMA MAELEKEZO
Bonyeza hi "Soma Kitabu" kisha itakupeleka kwenye fomu yaku login, hakikisha ume login na namba uliyojiunga nayo ndipo utaendelea sasa kusoma kitabu chote